Dully Sykes Salome Lyrics

KIITIKIO

Oh oh oh...!
Salome juu ya kaburi lako nalia aaa!
Kilio nakisikia, dakika za mwisho
Mpenzi w___u najutiaa kosa nilokufanyiaa
x2

(verse 1)
Siku ya kwanza nilikutana na wewe
Akili iliruka na kupata kiwewe
Sikuamini kama ningekutana na wewe
Hilo la kwanza naomba unielewe
Nikakutongoza ukanikubalia
Ulijipa moyo tena mia kwa mia
Umekwishapata bwana atakayekuoa
k__be nilikuona kama demu wa kuzugiaa
Miezi saba mbele iliendelea
Na mapenzi kwako we'yakapungua
k__be ulikuwa na mimba ya kujifungua
Miezi yote hiyo wala hukuniambia
Ulijua lazima nitaisaigia
Na ndio ndoto yangu hiyo ilikuwa
Na ulipojaribu mimi kuniambia
Katukatu nami nikakutalia
Salome mpenzi w___u ukaanza kulia
Kwa uoga w___u mimi nikakuambia
Tuonane siku inayofuatia
Kwa unyonge Salome ukaitikia

KIITIKIO

(verse 2)
Siku ya pili tena ilipofikia
Asubuhi mapema ni-nikakimbia
Nikakimbia kuelekea Mbeya
Huku nyuma Salome uliningojea
Saa dakika, sekunde zilipotokea
Ulichoka mpenzi kwa kuningojea
Ikabidi uje kuniulizia
Nyumbani wakesema Dully ameshakimbia
Salome mpenzi w___u ulinyong'onyea
Hazikupita dakikaa ukazimia
Ndoo za maji tatu wakakumwagia
Ndipo hapo fahamu zikakurudia
Ulilia mwishowe mpaka kujutia
Ulijuta kwa nini ulikunikubalia
Ulirudi nyumbani kwenu unalia
Hadi chumbani kwako ukajifungia
Salome mpenzi w___u ukaandika barua
"Msifunge Dully mimi najiua"
Dakika tano mbele zilipowadia
Polepole kitanzi ukajifungia
Ukajinyonga na kuiaga dunia
Nisamehe Salome leo najutia
Ukajinyonga na kuiaga dunia
Nisameheee Salome leo najutia

KIITIKIO x2

See also:

70
70.56
Allan Theo Jamais Lyrics
Fergie Fergielicous Lyrics